Wednesday, March 9, 2011

Siku ya wanawake Duniani

Kwa upande wa Tanzania bado kuna changamoto kubwa kwa wanawake kuwa na nguvu.
Tarehe 08-03-2011 nilialikwa katika kipindi cha tuongee asubuhi, niliwapa wanawake changamoto na kuwaasa wawe wamoja kwani fimbo ya mnyonge ni umoja, nikafafanua wanavyochukiana na kubaguana.....mfano, katika vitengo vya utendaji hasa hosptali, wanawake wanakuwa na furaha sana endapo katika vitengo hivyo wanapewa madaktari wa kiume, ila wakiwepo madaktari wa kike utasikia lawama na kashifa nyingi...pia nikawaonya wasiingize siasa katika umoja wao kwani ukitazama chama hicho sasa kina mwelekeo wa kisiasa, angalia mwenyekiti wao wa taifa ni mke wa rais ccm,katibu mbunge ccm n.k, pia wakatae mfumo wa viti maalum vya ubunge, kwani wao wanasema wanaweza, hivyo wanatakiwa kudhihirisha uwezo wao na wapambane na unyonge wao.

No comments: